VIRUTUBISHO VINAVYOPATIKANA KATIKA NYAMA NYEUPE
Imewekwa: 12 Apr, 2023

Nyama nyeupe kama vile kuku na bata mzinga, hiki ni chanzo kizuri na virutubisho muhimu amabvyo ni muhimu kwa afya na ukuaji kwa ujumla.

Hapa tutaelezea baadhi ya virutubisho muhimu vinavopatikana kwenye nyama nyeupe:

  • PROTINI: nyama nyeupe ni chanzo kizuri cha protini bora amabayo ni muhimu kwa kujenga mwili na kurekebisha tishu za misuli.
  • MADINI YA SELENIUM: nyamanyeupe ni chanzo kizuri na madini ya seleniamu, ni muhimu kwa tezi ya thairoidi, ufanyaji kazi ya mwilini ulinzi wa antioxidant
  • NIASIN: nyama nyeupe ni chanzo kizuri cha niasin na amabyo ni muhimu kwa uzalishaji wa nishati mwilini, kurekebisha vinasaba na ufanyaji kazi wa mfumo wa neva.
  • VITAMINI B6: nyama nyeupe ni chanzo muhimu cha vitamini B6, ni muhimu kwa uzalishaji wa chembe nyekundu za damu, ufanyaji kazi wa mfumo wa neva, inasaidia mwili kuvunja vunja protini, vyakula vya wanga na mafuta ndani ya mwili.
  • MADINI YA PHOSPHORASI: nyama nyeupe ni chanzo kizuri cha madini ya phosphorasi ambayo ni muhimu kwa afya ya mifupa, uzalishaji wa nishati mwilini ma uzalishaji wa vinasaba
  • ASIDI YA PANTOTHENIC (VITAMINI B5): nyama nyeupe ni chanzo kizuri cha vitamini B5 ambayo ni muhimu kwa uzalishaji wa homoni na mwili kuvunja vunja virutubisho vya protini, wanga na mafuta mwilini
  • MADINI YA POTASHIAMU: nyama nyeupe ni chanzo bora cha madini ya potashiamu ambayo ni muhimu kwa kazi za misuli na neva za mwili, kurekebisha presha ya damu na afya ya mifupa.

Ni muhimu kuzingatia kuwa mikato tofauti ya nyama nyeupe ina kuwa viwango tofauti vya virutubisho, ni muhimu kuchagua mikato ya nyama isiyo na mafuta na kula kwa kiasi kuepuka ulaji mkubwa wa mafuta na lehemu zilizopo kwenye nyama. Kwa kuongezea, ni muhimu kupika nyama kwa usahihi na kuiva vizuri kuhakikisha usalama wa chakula na kuzuia uwepo/kutokea kwa vimelea hatarishi vinavyoweza kuongezeka kwa magonjwa sugu.