1. UTANGULIZI
Tasnia ya nyama hapa nchini inasimamiwa na Sheria ya Nyama Na. 10 ya Mwaka 2006. Sheria hii ilitungwa kutokana na kuwepo kwa ombwe katika usimamizi wa tasnia ya nyama baada ya kuvunjwa kwa mamlaka ya kusimamia na kuendeleza mifugo na mazao yake (Livestock Development Authority - LIDA) mwanzoni mwa miaka ya 1980. Vile vile kumekuwepo na hitajio la nyama bora na salama katika soko la ndani na nje ya nchi.
Ili kusimamia utekelezaji wa sheria ya Nyama Na. 10 ya Mwaka 2006 Bodi ya Nyama Tanzania iliundwa chini ya kifungu 9 (1) kwa lengo la kuweka misingi thabiti ya kuendeleza uzalishaji, usindikaji, biashara ya mifugo, nyama na mazao yake inayozingatia ubora na viwango ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi. Aidha, katika kutekeleza majukumu hayo Bodi haina budi kushirikiana na wadau mbalimbali zikiwemo Mamlaka za Serikali za Mitaa, hivyo Bodi imeandaa kanuni na miongozo ya ukaguzi, upangaji wa madaraja ya mifugo na nyama na usajili wa wadau wa tasnia ya nyama ili kuelekeza wadau katika kutekeleza majukumu yao kwa mujibu ya sheria. Ili kutekeleza usajili ni dhahiri kuwa ukaguzi ndio ufunguo wa utambuzi na usajili wa wadau wa Tasnia ya Nyama.
2.USAJILI WA WADAU WA TASNIA YA NYAMA
2.1 Lengo la Usajili
Kuwezesha wadau kushiriki kikamilifu katika kuendeleza tasnia ya nyama kuanzia kwenye uzalishaji, usindikaji, biashara ya mifugo, nyama na mazao yake. Vile vile inawezesha wadau kupatiwa huduma mbalimbali zikiwemo taarifa muhimu za tasnia na kuunda mtandao baina yao.
2.2 Wadau na Maeneo Yatakayosajiliwa
Watakaosajiliwa na kutambuliwa ni watu binafsi, taasisi, vyama vya kijamii kampuni na maeneo yanayotumika katika uzalishaji wa mifugo, katika hatua mbalimbali za mnyororo wa thamani wa zao la nyama kibiashara. Wadau na maeneo hayo ni pamoja na:-
3. VIGEZO VYA USAJILI
3.1 Mfugaji/Mmiliki wa shamba la mifugo
3.2Minada ya Mifugo
3.3 Msimamizi wa Mnada
3.4 Dalali
3.5 Mfanyabiashara wa Mifugo hai ndani na nje ya nchi
3.6 Vyama na Vikundi vya Wadau
Vyama vitakavyosajiliwa ni pamoja na vyama na vikundi vya wafugaji, wafanyabiashara, wasindikaji, walaji, wauza pembejeo, wauzaji na waangizaji nyama, bidhaa zake na pembejeo nje ya nchi.
Vyama hivyo vinatakiwa kuwa na sifa zifuatavyo:-
3.7 Wadau wengine watakaotambuliwa
Wadau wengine na maeneo yao wanaotakiwa kutambuliwa ni pamoja na:-
3.8 Utaratibu wa Kusajili
Utaratibu wa kusajili wa wadau na maeneo ya uzalishaji mifugo utazingatia mambo yafuatayo:-
S.L.P 1344 DODOMA,
Area D, Mtaa wa Ndugai,
Barabara ya Magufuli
Nukushi : Simu : +255734210199 Barua pepe : barua@tmb.go.tz
Copyright ©2017 Tanzania Meat Board . All rights reserved.
Designed and Developed by e-Government Authority (eGA). Inaendeshwa na TMB.