Bw. IMANI PAULO SICHALWE
Science in Tropical Animal Production
Bwana Imani Paulo Sichalwe, ni Mtaalam katika sayansi ya wanyama mwenye Shahada ya Uzamili katika Uzalishaji wa wanyama katika ukanda wa kitropiki (Mbobezi katika Sayansi ya Nyama ) kabla ya hapo alikuwa na shahada ya Sayansi katika Sayansi ya Wanyama aliyoipata katika Chuo Kikuu cha Kilimo-Morogoro Sokoine.
Hivi sasa, anafanya kazi ya Kaimu Msajili wa Bodi ya Nyama Tanzania iliyopo chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi. Kabla ya kuchaguliwa kwake, alishawahi kufanya kazi ya Ualimu katika Shule ya Sekondari ya Pugu muda wa mwaka mmoja na alikuwa Mkufunzi Mwandamizi wa Mifugo huko LITA-Tengeru, Arusha kwa miaka 12 mpaka alipopata uteuzi wa kuwa Kaimu Msajili wa Bodi ya Nyama Tanzania.
Mbali na kiwango cha elimu na uzoefu uliotajwa hapo juu, pia amehudhuria warsha kadhaa za kujenga uwezo zikiwa ni pamoja na – Matumizi ya Majedwali ya Mchanganyo wa vyakula vya mifugo na matumizi yake kama ilivyowezeshwa na ASARECA katika Chuo Kikuu cha Kilimo - SOKOINE, Mafunzo ya muda mfupi juu ya mbinu za ufundishaji na kupewa cheti cha (TOT) kama yalivyowezeshwa na ADEM-Bagamoyo, mafunzo ya muda mfupi juu ya ufanisi wa Maendeleo ya Uchumi Vijijini juu ya Kilimo, mafunzo yaliyofanyika LITA-Tengeru na kuwezeshwa na RECODA TZ, mafunzo na kupewa cheti juu ya utunzaji wa Ng’ombe wa maziwa na uzalishaji kama yalivyowezeshwa na COCHRAN nchini Amerika ya Kaskazini, mafunzo na kupewa cheti juu ya Usimamizi wa Taasisi na Mipango ya Biashara (INTERNATIONAL) yaliyofanyika nchini Uingereza.
.
S.L.P 6085 DSM,
Veterinary Complex
131 Barabara ya Nelson Mandela,
Nukushi : Simu : +255734210199 Barua pepe : info@tmb.go.tz
Copyright ©2017 Tanzania Meat Board . All rights reserved.
Designed and Developed by e-Government Authority (eGA). Inaendeshwa na TMB.